Auawa baada ya kujaribu kuiba helikopta ya polisi Marekani
HILLSBORO- MTU mmoja amepigwa risasi na kufa, baada ya
kuruka uzio na kujaribu kuiba helikopta ya polisi mjini hapa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Koin TV mjini Portland, ilieleza
kuwa mtu huyo aliyevalia kinyago cha kuficha sura, aliruka uzio na kuingia
kwenye sehemu ya maegesho ya helikopta hizo akiwa na mwanafunzi wa urubani.
Mara baada ya kufanikiwa kuingia, aliwanyooshea silaha askari na kufyatua
hewani risasi moja kabla ya kujaribu kutoroka kwa kuruka tena uzio na kuanza
kukimbia.
Hata hivyo, mshukiwa huyo hakuweza kwenda mbali kwani alipigwa risasi na
kufariki wakati akipatiwa huduma ya kwanza na askari walinzi wa eneo hilo.
CBS
No comments