Header Ads

Waliooa wanawake wengi washtakiwa Canada



Winston Blackmore the religious leader of the polygamous community of Bountiful, B.C. shares a laugh with six of his daughters and some of his grandchildren, in this April 21, 2008 photo.
Kiongozi wa kidini Canada, Winston Blackmore ambaye anadaiwa kuwa na watoto zaidi ya 145 na wanawake 24.

OTTAWA- VIONGOZI wawili wa dini nchini, wamepatikana na hatia ya kuoa wake wengi.
Mahakama iliambiwa kuwa, Winston Blackmore mwenye umri wa miaka 61 alioa wanawake 24, huku mkwe wake James Oler akioa wanawake watano.
Wote walipatikana na hatia ya shtaka moja la kuwaoa wanawake wengi na kila mmoja anakabiliwa na kifungo cha miaka mitano jela.
James Oler arrives at the BC Supreme Court in Cranbrook, British Columbia
James Oler ambaye naye anadaiwa kuwa na wake watano.
Hukumu hiyo, imetajwa kuwa mtihani mkubwa kwa uhuru wa kidini nchini Canada. Blackmore na Oler wanatoka katika jamii moja ya dini, inayodaiwa kuwa na waumini 1,500 ambayo ilianzishwa mwaka 1946.
Wote walikuwa ni makasisi wa dhehebu lililojitenga, kutoka kanisa la Fundamentalist Church of Jesus Christ of Latter-Day Saints (FLDS). Blackmore alifukuzwa kutoka FLDS mwaka 2002 na mahala pake pakachukuliwa na Oler.
Matawi ya dhehebu hilo yako nchini Marekani, ambako kuna wanachama karibu 10,000. Kuoa wanawake wengi ni haramu chini ya sheria za Canada na Polisi walianza kuchunguza dhehebu hilo kuanzia miaka ya 1990.
BBC.

No comments

Powered by Blogger.