Header Ads

Marekani; Korea Kaskazini iko mbioni kujaribu kombora lingine



http://botapress.info/wp-content/uploads/2017/04/rrr_1492448161-5499741.jpg

SEOUL- KWA mujibu wa habari za kiintelijensia kutoka Idara ya Mambo ya Ndani ya Marekani, Korea Kaskazini kwa sasa inajiandaa kufanya majaribio ya kombora lingine ambalo bado halijajulikana.
Maofisa wa idara hiyo, wanadai kuwa wamebaini kuwasili kwa magari yanayobeba vifaa vya kujaribia makombora, katika eneo la Kusong lililo Kaskazini mwa taifa hilo tangu Ijumaa ya wiki iliyopita.
Aidha, maofisa hao wanadai kuwa vifaa hivyo vinapoonekana kwenye eneo hilo basi jaribio lazima lifanyike ndani ya siku sita. Pia, inadaiwa kuwa huenda ni maandalizi kwa ajili ya kujaribu kombora siku ya Julai 27, ambayo ni maadhimisho ya Makubaliano Matukufu yaliyomaliza vita baina ya Korea Kaskazini na Kusini.
Jumatano ya wiki iliyopita, Shirika la Habari la CNN liliripoti kuwa wanaintelijensia wa Marekani wamebaini uwepo wa maandalizi ya jaribio la kombora lingine la aidha kutoka bara moja hadi jingine (ICBM) au kombora la masafa mafupi.
Maofisa wawili walisema kuwa, satalaiti ya Marekani ilionesha picha hizo na rada kwenye satalaiti hiyo ilionesha uwezekano wa taifa hilo kufanya jaribio hilo.
Eneo la Kusong limekuwa maarufu kwa majaribio ya makombora, ambapo Mei mwaka huu walifanya jaribio la kombora la masafa mafupi la KN-17 ambalo limesafiri kwa maili 500 kabla ya kutua Mashariki mwa bahari ya Japan.
CNN

No comments

Powered by Blogger.