Header Ads

Mezani Asubuhi; Conte amwagiwa noti Chelsea # Renato Sanches ruksa Man Utd # Sanchez kununua mkataba wake Arsenal



http://video.skysports.com/IyZjZiYjE63J9UDKgSG8M_0L4WaFMaoL/promo319786847

LONDON- KOCHA wa Chelsea, Antonio Conte amepewa fungu jipya la pauni milioni 150 (sh bilioni 435) kwa ajili ya kutumia kwenye zoezi la usajili msimu huu.
Katika orodha yake kuna majina ya Virgil van Dijk wa Southampton, Alex Sandro wa Juventus, Antonio Candreva wa Inter Milan, Tom Davies wa Everton na Fernando Llorente wa Swansea City. Daily Mirror.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict0003399687001.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Carlo Ancelotti ameiambia Manchester United kuwa, wanaweza kumsajili kiungo wa Bayern Munich na Ureno, Renato Sanches (19) lakini wasahau kuhusu mpango wao wa kumsajili Arturo Vidal (30) kwani hauzwi. Independent.
https://static.standard.co.uk/s3fs-public/styles/article_small/public/thumbnails/image/2017/05/26/12/alexissanchez.jpg
Winga wa Arsenal, Alexis Sanchez (28), yuko tayari kulipa fedha kwa ajili ya kununua mkataba wake ili aruhusiwe kujiunga na Manchester City. Pia, raia huyo wa Chile anasakwa na Juventus ya Italia. Independent.
http://images.performgroup.com/di/library/GOAL/f3/b5/hd-neymar-barcelona-icc_bkxu7y255kqg1ximnsbzswaz1.jpg?t=1823806901
PSG imesema itamtoa kiungo wao, Marco Verratti (24) na pauni milioni 90 (sh bilioni 261), kwa Barcelona ikiwa ni sehemu ya usajili wa mshambualiji raia wa Brazil, Neymar (25). Diario Gol.
http://cdn.images.dailystar.co.uk/dynamic/58/photos/464000/620x/56781f3ebb015_GettyImages500068290.jpg
Roma ya Italia, imeweka mezani dau la pauni milioni 30 (sh bilioni 87) kwa ajili ya kumsajili winga wa Leicester City, Riyad Mahrez (26) lakini klabu hiyo maarufu kama Mbweha, wanataka pauni milioni 50 (sh bilioni 145). Daily Mail.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/03/nintchdbpict000299479451.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Everton inaamini kuwa dau lao la pauni milioni 45 (sh bilioni 130.5), litakubaliwa na Swansea, kama ada ya uhamisho wa kiungo wao, Gylfi Sigurdsson (27) na kukamilisha usajili huo ifikapo Alhamis wiki hii. Daily Mail.
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2016/01/30/17/30BA457000000578-3424330-image-a-30_1454175062765.jpg
Klabu ya Galatasaray inahusishwa na mpango wa kumnunua kiungo wa Arsenal na Misri, Mohamed Elneny (25). Fotospor.
http://cdn3-i.hitc-s.com/454/celtics_moussa_dembele_celebrates_scoring_their_third_goal_332899.jpg 
Marseille inafanya mazungumzo na klabu ya Celtic ya Scotland, kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wao kinda, Moussa Dembele (20) kwa dau la pauni milioni 20 (sh bilioni 58). Daily Express.
http://20.theladbiblegroup.com/s3/content/808x455/ea4dd8e9591ab77cb1370a43d6202e00.png
Borussia Dortmund wanataka kumsajili winga wa Man City, Jadon Sancho (17), ambaye hatima yake iko shakani klabuni hapo kutokana na kutosainishwa mkataba. ESPN.
http://i2.mirror.co.uk/incoming/article9798223.ece/ALTERNATES/s615/Arsenal-v-Hull-City-Premier-League.jpg
Mshambuliaji wa Arsenal, Lucas Perez anataka kuondoka klabuni hapo kutokana na kuhisi kuwa hatendewi haki. Hiyo inakuja baada ya klabu hiyo kumsajili Alexandre Lacazette na kumpa jezi namba 9 aliyokuwa akiitumia yeye (Perez). Daily Telegraph.

No comments

Powered by Blogger.