Urusi yajibu vikwazo vya Marekani
![https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/14BA5/production/_97110948_gettyimages-630672230.jpg](https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/14BA5/production/_97110948_gettyimages-630672230.jpg)
MOSCOW- WAKATI Bunge la Senate la Marekani kuidhinisha
muswada wa vikwazo vipya, Urusi imelitaka taifa hilo kupunguza watumishi wake wa
ubalozi mjini hapa hadi kufikia 455.
Aidha, Urusi
imesema imetwaa baadhi ya miundombinu inayotumika kwenye shughuli za kibalozi
kama Marekani ilivyofanya mwaka jana. Mwaka jana, Marekani ilitaifisha majengo
mawili ya Urusi, yaliyokuwa yakitumika katika shughuli za kibalozi nchini humo.
Hata hivyo,
uamuzi wa Urusi unatarajiwa kutozuia vikwazo vingine ambavyo vimewekwa na
Marekani kwa madai kuwa Urusi kulitwaa kinguvu jimbo la Crimea la Ukraine mwaka
2014.
Pia, kumekuwa
na uchunguzi unaoendelea iwapo Urusi imeingilia uchaguzi wa taifa hilo
uliofanyika mwaka jana.
BBC.
No comments