Header Ads

Mezani Jioni; Barca kutoa £81m na Rakitic Liverpool # Neymar azichapa mazoezini # Sanchez kuchelewa mazoezi Arsenal



http://d.ibtimes.co.uk/en/full/1471020/ivan-rakitic.jpg

BARCELONA- BARCELONA wamesema wapo tayari kutoa pauni milioni 81 (sh bilioni 234.9), pamoja na kiungo wao, Ivan Rakitic ikiwa ni sehemu ya dili la uhamisho wa Philippe Coutinho kutoka Liverpool kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa La Liga. 

https://static.independent.co.uk/s3fs-public/styles/article_small/public/thumbnails/image/2017/07/25/13/neymar.jpg
Sakata la usajili wa mshambuliaji wa Barcelona, Neymar, limezidi kuchukua sura mpya, baada ya mchezaji huyo kuahirisha safari ya kwenda China kukutana na mashabiki wake. Pia, Neymar alisababisha mazoezi ya timu hiyo kuvunjika kutokana na kugombana na mchezaji mwenzake. 

http://video.skysports.com/VtMnIzMDE6DhRsVXtwLZFTRWYEXtSRQg/promo276689804
Wakala wa Gareth Bale, Jonathan Barnett amepuuza ripoti zinazodai kuwa mteja wake ataondoka Real Madrid ni upuuzi mtupu. Barnett amedai Bale hawezi kuondoka Real Madrid. Hata hivyo, kocha wa Madrid, Zinedine Zidane alisema lolote linaweza kutokea msimu huu wa usajili.

https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/05/683893852.jpg?w=748&h=467&crop=1
Alexis Sanchez ambaye alitarajiwa kurejea mazoezini Jumapili ijayo, sasa anaweza kuchelewa zaidi, baada ya kupost picha yenye maelezo kwamba anaumwa. Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger alitarajia kuwa Sanchez atajiunga na wenzake mwishoni mwa wiki. 

https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/07/820669942.jpg?w=748&h=498&crop=1
Mwenyekiti wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge amesema kocha wa Chelsea, Antonio Conte ameulizia kuhusu upatikanaji wa kiungo Renato Sanches. Hata hivyo, Rummenigge ameeleza kuna timu 10 zinazomhitaji mchezaji huyo.

https://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2015/10/24/11/Pep-Guardiola.jpg
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amesema anatamani kuongeza mkataba na timu hiyo lakini hatima yake klabuni hapo itaamuliwa na idadi ya vikombe atakavyotwaa msimu ujao.

https://www.whufc.com/sites/default/files/inline-images/ChicharitoShirt726.jpg
Mchezaji mpya wa West Ham, Javier Hernandez ‘Chicharito’ amesema alilazimika kuzipiga chini ofa kutoka Hispania na Italia, ili aweze kurudi kwenye ligi bora ya England maarufu ‘EPL’.

http://i2.chroniclelive.co.uk/incoming/article13399060.ece/ALTERNATES/s1227b/Newcastle-United-Unviel-New-Signing-Mikel-Merino.jpg
Kocha wa Newcastle United, Rafael Benitez amesema anajisikia vema baada ya kufanikiwa kumsajili kinda kutoka Borussia Dortmund, Mikel Merino kwani ni mmoja kati ya viungo bora vijana.
Sky Sports.




No comments

Powered by Blogger.