Ukuaji wa uchumi China wafikia asilimia 6.9
HONG KONG- TAKWIMU za Uchumi, zinaonesha kuwa uchumi wa China
ulikua kwa asilimia 6.9 kati ya Aprili na Juni na kuvuka matarajio ya wengi
ambao awali hawakuweka kadiro hilo.
Ukuaji huo
ambao ni mkubwa ukilinganishwa na miezi mitatu iliyopita, ulikuwa sawa na robo
ya kwanza ya mwaka 2017.
Wachanganuzi
wengi, walitarajia kuwa uchumi wa China huenda ukapunguza kasi ya ukuaji wake. Lakini,
takwimu za hivi punde ziko juu kuliko matarajio ya ukuaji wa asilimia 6.5.
Licha ya
jitihada za kupunguza uwekezaji katika nyumba, uwekezaji katika sekta za ujenzi
ulikua kwa asilimia 8.5 katika robo ya kwanza ya mwaka, ambayo ni juu kutoka
kipindi kama hicho mwaka 2016.
Wadadisi
wanatabiri kuwa sheria ngumu za ukopeshaji haziwezi kuathiri uwekezaji kama
wengi walivyotarajia.
BBC
No comments