Sitashiriki mdahalo wa wagombea wenza kwani sijaalikwa- Ruto
NAIROBI-
NAIBU Rais nchini, William Ruto, amesema hatohudhuria mdahalo wa wagombea wenza
ambao unafanyika leo kwa kuwa hajawahi elezwa kuhusu jambo hilo wala kualikwa.
Mdahalo huo
baina ya Ruto, mpinzani wake ambaye ni mgombea mwenza kutoka Muungano wa NASA,
Kalonzo Musyoka na wengine kutoka vyama vingine, ulitarajiwa ufanyike kwenye
ukumbi wa Chuo Kikuu cha Katoliki cha Afrika Mashariki jijini hapa.
“Nimeshangazwa
sana kutokana na kuwa, hakuna hata mtu mmoja aliyenishirikisha kwenye jambo
hilo (mdahalo). Kiutaratibu, ilihitajika niambiwe kuhusu tarehe, muda, taratibu
za ushiriki na sheria zake na mambo mengineyo,” alisema Ruto.
Kiongozi huyo
alisema kuwa, si uungwana kusikia kuwa kuna mdahalo huo kwenye vyombo vya
habari na mitandao ya kijamii.
The Star.
No comments