Header Ads

Ujio wa Lacazzette utamshawishi Sanchez kubaki Arsenal



Alexandre Lacazette was the second top scorer in Ligue 1 last season with 28 goals
LONDON- UJIO wa mshambuliaji wa kati, Alexandre Lacazzette ambaye jana alikamilisha vipimo vya afya katika klabu ya Arsenal, huenda ukambakiza klabuni hapo Alexis Sanchez.

Kwa mujibu wa mmoja wa wachambuzi nguli wa soka Uingereza, Nigel Winterburn, ujio wa Lacazzette unatarajiwa kuhuisha ndoto za Arsene Wenger kumbakiza Sanchez klabuni hapo ili asaidiane kazi na mshambuliaji huyo kutoka Ufaransa.
“Ninafikiri iko wazi kwa mashabiki wa Arsenal na hata kwake Wenger kuwa, sehemu ya muhimu zaidi ya kuiongezea nguvu ni safu ya mbele ya timu hiyo,”
“Hivyo natumaini kuwa Giroud atabaki, kwani nafikiri bado ni mtu anayehitajika kwenye timu. Arsenal wanafahamu kuwa, wanahitaji wachezaji bora ili kuwasaidia kupambana kwa ajili ya ubingwa”
“Na kwa namna yoyote ile, Sanchez atashawishika kubaki na atakuwa akicheza winga ya kushoto au kulia ama nyuma ya mshambuliaji. Kwa pamoja wataing’arisha Arsenal, hivyo hawawezi kwa namna yoyote kumnunua Lacazzette kwa pauni milioni 52 na kumwachia Sanchez aondoke ndani ya wiki mbili zijazo,” alisema Winterburn.
Sky Sports

No comments

Powered by Blogger.