Uingereza yadai Saudi Arabia inafadhili wenye misimamo mikali ya kidini

LONDON-
RIPOTI Mpya na taasisi ya Henri Jackson Society, imeeleza kuwa Saudi Arabia ndiyo
mfadhili mkuu wa watu wenye misimamo mikali ya kidini nchini.
Ripoti hiyo imesema
kuwa, kuna ushirikiano wa wazi kati ya mashirika ya Kiislamu yanayotoa ufadhili
kwa wahubiri wenye chuki na makundi ya kijihad yanayokuza ghasia.
Idara ya Mmambo
ya Nje ilitaka kuchunguzwa kwa jukumu la Saudi Arabia na mataifa mengine ya
Ghuba. Ubalozi wa Saudia nchini, umesema kuwa madai hayo ni ya ‘uongo’.
Mawaziri
wanakabiliwa na shinikizo ya kuchapisha ripoti ya makundi ya Kiislamu yaliyoko
nchini.
Ripoti hiyo
ya Idara ya Mambo ya Ndani, kuhusu uwepo wa makundi ya kijihad iliyoanzishwa na
aliyekuwa Waziri Mkuu, David Cameron mwaka 2015, bado haijakamilika na kuna
ripoti za iwapo itachapishwa au la.
Wakosoaji
wanasema kuwa huenda ikawa vigumu kwa Serikali kuisoma, kutokana na ushirikiano
wa karibu wa kidiplomasia, usalama, kiuchumi na mataifa ya Ghuba hususan Saudi
Arabia.
Ripoti hiyo
ya leo, inasema kuwa mataifa kadhaa ya Ghuba ikiwemo Iran yanatoa ufadhili wa
kifedha kwa misikiti na taasisi za elimu ya Kiislamu ambazo zimekuwa zikiwakuza
wahubiri wa chuki, suala linalosababisha kuenea kwa Itikadi kali.
Katika
kilele cha orodha hiyo, ripoti hiyo inasema ni Saudia. Inadai kwamba, watu
binafsi na wakfu wamehusishwa kueneza itikadi za Wahabby ikinukuu mifano kadhaa.
Katika visa
vingine vichache, ripoti hiyo inadai taasisi nchini zinazopokea ufadhili wa
Uingereza zinatekeleza operesheni zake moja kwa moja kutoka Saudia, ijapokuwa
fedha hizo huonekana kununua ushawishi wa wafadhili wa kigeni.
Katika
taarifa yake ubalozi wa Saudia mjini hapa, unasema kuwa tuhuma zozote kwamba
ufalme huo unafadhili watu wenye itikadi kali, hazina msingi na wala ushahidi
wowote.
Imesema kuwa
taifa hilo limeshambuliwa na Al-Qaeda na wapiganaji wa Islamic State.
Imeongezea
kwamba: “Hatuungi mkono na hatuwezi kuunga mkono vitendo vya makundi yenye
itikadi kali, na hatutapumzika hadi makundi hayo yaliokosa mwelekeo na
mashirika yao yaangamnizwe.”
BBC
No comments