Header Ads

Boko Haram waua na kuteka wanawake Niger



Image result for Boko Haram
NIAMEY- KUNDI la wanamgambo wa Kiislamu la Boko Haram, limedaiwa kuua watu tisa na kujeruhi watu kadhaa na kuteka wengine wanaokadiriwa kufikia 40 katika kijiji cha NGalewa kilichopo Mashariki mwa mji wa Diffa nchini.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Adam Babakarna, alisema kuwa wanamgambo hao waliwasili kijijini hapo Jumapili jioni kwa kutumia ngamia na farasi na kisha kuanza kutekeleza unyama huo.
Babakarna alisema kuwa wengi wao wa waliochukuliwa mateka na wanamgambo hao, ni wanawake na watoto na kutishia kuwashikilia hadi hapo wapiganaji wenzao watakapoachiliwa na Serikali.
“Wapiganaji wanaoaminiwa kuwa ni Boko Haram, wameua watu tisa kwa kuwachinja na kisha kuondoka na wanawake wapatao 37. Vyombo vya ulinzi tayari vinafuatilia tukio hilo kwa ukaribu,” alisema Gavana wa Diffa, Laouali Mahamane Dan Dano wakati alipokuwa akizungumza na televisheni ya Serikali. 
Aidha, Dan Dano alisema kuwa anatumai kuwa vyombo hivyo vitabaini maficho ya wanamgambo hao na kisha kuwakomboa wanawake hao.

CBS News

No comments

Powered by Blogger.