Header Ads

Tottenham haiuzwi na wala haina mpango wa kuuzwa



Tottenham Hotspur's English midfielder Dele Alli (C) kicks the ball during the friendly football match between Tottenham Hotspurs and Kitchee FC
LONDON- UONGOZI wa klabu ya soka ya Tottenham Hotspurs iliyopo London Kaskazini, umesema kwamba timu hiyo haiuzwi na hakuna mpango wowote wa kuiuza.

Taarifa iliyotolewa na Bodi ya timu hiyo, ilieleza kuwa klabu hiyo haiuzwi na wala hakuna mpango wa kuiuza; “Bodi haipo kwenye mazungumzo ya aina yoyote yale yenye lengo la kuiuza klabu.”
“Bodi inaamini kuwa (makubaliano ya ufadhili wa uwanja huo), ilikuwa ni suluhisho tosha kwa matakwa ya mashabiki, waajiriwa na washika dau na kwa maendeleo ya klabu hii.”
Hayo yanajiri baada ya vyombo vya habari kudai kuwa, kampuni ya Iconiq Capital iko tayari kuinunua klabu hiyo ambayo msimu uliopita ilishika nafasi ya pili Ligi Kuu ya Uingereza nyuma ya mabingwa, Chelsea.
Habari hizo zinakuja wakati Tot wakiuhama uwanja wao wa White Hart Lane na kuhamia Wembley ili kupisha ujenzi. Tayari benki tatu za Bank of America Merrill Lynch International Ltd, Goldman Sachs Bank USA na HSBC Bank zimekubali kufadhili ujenzi huo.
BBC Sport

No comments

Powered by Blogger.