Header Ads

Jinamizi la moto lazidi kuiandama London



http://a57.foxnews.com/images.foxnews.com/content/fox-news/world/2017/07/09/camden-lock-market-fire-erupts-in-popular-london-tourist-destination/_jcr_content/par/featured_image/media-0.img.jpg/876/493/1499653587516.jpg?ve=1&tl=1
LONDON- JINAMIZI la moto limezidi kuiandama Uingereza, baada ya moto mkubwa kuzuka ghafla katika soko la Camden Lock Market na kusababisha hasara kubwa.

Zaidi ya watumishi 70 na injini 10 za kuzimia moto kutoka katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, zilitumika kupambana na moto huo mkubwa ambao ulizuka majira ua 2:50 alfajiri (kwa saa za Uingereza).
Licha ya moto huo kuwa mkubwa, Kikosi cha Zimamoto cha London kimeeleza kuwa hakukuwa na mtu yeyote aliyejeruhiwa.
Moto huo ambao bado chanzo chake hakijajulikana, unakuwa wa pili kuteketeza soko hilo baada ya ule wa kwanza uliotokea mwaka 2008 na kusababisha hasara.
Soko hilo linadaiwa kutembelewa na watu zaidi ya milioni 28 kila mwaka, wengi wao wakiwa wanaenda kufanya manunuzi huku wengine wakienda kufanya utalii sokoni hapo.
ABC News

No comments

Powered by Blogger.