Header Ads

Tetesi za usajili leo; Everton yamwinda Rooney, #Mourinho akereka Man United, #Arsenal ikiwawinda ‘pacha’ wa Sporting Lisbon ya Ureno



https://ichef.bbci.co.uk/live-experience/cps/800/cpsprodpb/vivo/live/images/2017/7/4/d4fbea3f-5e46-40c5-aa4c-43ff36d456fa.jpg
Wayne RooneyWayne RooneyWayne Rooney
LONDON- KWA mujibu wa ripoti maalum ya wavuti ya michezo ya Talksport, imebainika kuwa klabu ya Everton inafanya kila liwezekanalo ili kumsajili mshambuliaji wa timu ya Manchester United na Uingereza, Wayne Rooney, msimu huu.

Hatua hiyo ni sawa na kumrudisha mshambuliaji huyo nyumbani, kwani maisha ya mpira ya Rooney yalianzia hapo Goodson Park kabla ya kutimkia Man United mwaka 2004.
https://ichef.bbci.co.uk/live-experience/cps/800/cpsprodpb/vivo/live/images/2017/7/4/11e4eb73-969e-4c86-8999-368dfff927ec.jpg Jose Mourinho
Jose Mourinho
Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho (pichani) ameonekana kukerwa na kile alichokiita kuwa mwendo wa pole wa klabu hiyo kwenye suala la usajili wa wachezaji msimu ujao.
Licha ya kuwa tayari ana beki Victor Lindelof kutoka Benfica, bado Mreno huyo haridhishwi na spidi ndogo ya klabu hiyo kwenye usajili kwani wanachelewa kukamilisha dili la mshambuliaji Alvaro Morata kutoka Real Madrid na kiungo wa Chelsea, Nemanja Matic.
“Mtendaji Mkuu wa Man United, Ed Woodward mwishoni mwa mwezi uliopita, alisafiri kwenda New Zealand kuangalia mchezo wa rugby kati ya New Zealand na Uingereza. Kitendo hicho kimemstaajabisha Mourinho na wenzake klabuni hapo,” limeandika gazeti la The Guardian.
https://ichef.bbci.co.uk/live-experience/cps/800/cpsprodpb/vivo/live/images/2017/7/4/978496cf-61eb-4d5d-baae-139f571c13ad.jpg
Gazeti la The Telegraph limeandika kwamba, klabu ya West Ham United inahitaji huduma za mchezaji wa zamani wa Manchester United, Javier Hernandez (pichani) ambaye kwa sasa anakipiga Bayer Leverkusen ya Ujerumani.
Pia, klabu hiyo maarufu kama ‘Wagonga nyundo wa London’ inadaiwa wanawawinda Olivier Giroud wa Arsenal na Michy Batshuayi wa Chelsea.
Image result for Florian Lejeune
Wageni wenyeji wa Ligi Kuu ya Uingereza, Newcastle United tayari wamekamilisha dili la kumsajili beki kutoka Eibar ya Hispania, Florian Lejeune (26) kwa dau la pauni milioni 8.7 (sh bilioni 23.49).
Kocha wa Newcastle United, Rafael Benitez amesema kwamba; “Ni mchezaji ambaye amefanya vema nchini Hispania. Nimemfahamu tangu akiwa Villarreal. Amekuwa akiimarika mara kwa mara.”
Lejeune amesaini dili la miaka mitano katika klabu hiyo yenye makao makuu yake Tyneside.
http://www.scorehighlights.com/wp-content/uploads/2017/07/cdn.images.express.co_.ukWilliam-Carvalho-824284-8aef7e7d757a0aab48cf20119b90da60daea860a.jpg
The Sun linaripoti kuwa ‘Washika Bunduki wa London’ Arsenal, wamepanga kutumia pauni milioni 70 (sh bilioni 154) kuwanasa ‘pacha’ wawili kutoka Ureno.
Pacha hao ni, William Carvalho ambaye ni kiungo na mshambuliaji Gelson Martins kutoka katika klabu ya Sporting Lisbon. Pia gazeti hilo limedai kuwa, Arsenal wako karibu kabisa kumsajili mshambuliaji wa Olympic Lyon, Alexandre Lacazette.

No comments

Powered by Blogger.