Header Ads

Mtoto wa George Weah asaini mkataba wa miaka 3 na PSG



Timothy Weah ajiunga na PSG
PARIS- TIMOTHY Weah ambaye ni mtoto wa galacha wa mpira wa Liberia, George Weah, amesaini mkataba wa kuitumikia klabu ya PSG kwa miaka mitatu.

Timothy ambaye awali alikuwa kwenye timu ya watoto ya PSG, anafuata nyayo za baba yake ambaye aliwahi kuitumikia klabu hiyo ya PSG kwa muda wa miaka 4 kuanzia mwaka 1992 hadi 1995.
Mshambuliaji huyo wa miaka 17 ametia saini mkataba wa miaka 3 na PSG na kuhitimisha uvumi ambao umekuwepo kwa muda mrefu kwamba, kinda huyo huenda akasainishwa mkataba rasmi na timu hiyo.
Mnamo Septemba 2016, Timothy alifunga hat-trick katika ushindi wa bao 8-1 dhidi ya klabu ya Ludogorets katika mechi yake ya kwanza ya Uefa.
“Ni fahari kubwa kuendeleza pale baba alipoachia,” alisema Weah ambaye alizaliwa mjini New York na kujiunga na New York Red Bulls kabla ya kujiunga na chuo cha mafunzo ya soka cha PSG mnamo Julai 2014.
“Niko katika klabu kubwa na natumai nitaendelea kuimarika ili niweze kuichezea timu kubwa,” alisema Timothy.
BBC

No comments

Powered by Blogger.