Header Ads

Asubuhi Njema; Mourinho ataka fedha na Kroos kwa De Gea # Chelsea wamtaka Aguero # Wenger akata tamaa kwa Mbappe



http://www.thehardtackle.com/wp-content/uploads/2012/03/De-Gea.jpg


LONDON- KOCHA wa Man United, Jose Mourinho amesema dili lolote kutoka Real Madrid kwa kipa wake, David de Gea (26), lazima lihusishe fedha na kiungo, Toni Kroos (27). Sun.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/02/nintchdbpict000303579200.jpg?strip=all&w=960
Baada ya kumsajili Tiemoue Bakayoko, Chelsea sasa imeelekeza nguvu zao kwa mshambuliaji wa Man City, Sergio Aguero (29) ilia je azibe pengo la Diego Costa ambaye ameambiwa anaweza kuondoka. Star.
http://static.goal.com/2733400/2733482_heroa.jpg
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger, amekata tamaa kuhusiana na mchakato wa kumsajili mshambuliaji wa Monaco, Kylian Mbappe (18) na badala yake ameelekeza nguvu zaidi kwenye usajili wa winga, Thomas Lemar (21) ambaye ameitaka Monaco imuuze kwa Arsenal. Telegraph.
http://i2.mirror.co.uk/incoming/article10140113.ece/ALTERNATES/s615/FC-Schalke-04-v-Borussia-Dortmund-Bundesliga.jpg
Borussia Dortmund wameongeza siku chache za kuendelea kusubiri ofa ya Chelsea kwa mshambuliaji wao, Pierre-Emerick Aubameyang (28). Mail.
http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/636/236/hi-res-97ab0048950936c0aac2743fb032c3b7_crop_north.jpg?1477926587&w=630&h=420
Chelsea imeeleza kuwa iko tayari kumpatia mkataba mnono wa miaka mitano, winga wa Ubelgiji na Atletico Madrid, Yannick Carrasco (23). Express.
https://static.standard.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2014/05/21/09/Ross%20Barkley%20stay.jpg
Tottenham Hotspurs wameongeza nguvu kwenye dili lao la kumsajili kiungo wa Everton, Ross Barkley (23), licha ya ofa yao ya awali kukataliwa. Everton pia wameripotiwa kudai kuwa, wako tayari kumuuza kiungo huyo. Independent.
http://e0.365dm.com/16/12/16-9/20/skysports-virgil-van-dijk_3860836.jpg?20161229154347
Beki wa Southampton, Virgil van Dijk (26) anaweza kusajiliwa na Liverpool, kwa dau la pauni milioni 60 (sh bilioni 174) na kuweka rekodi kwa klabu hiyo ya Anfield baada ya kudaiwa kutakiwa na Arsenal kwa dau la pauni milioni 45 (sh bilioni 130.5). Sun.
https://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2015/10/12/12/Alexis-Sanchez.jpg
Arsene Wenger ameeleza kuwa, ana matumaini ya kumshawishi mshambuliaji wake, Alexis Sanchez (28), ili aweze kubakia klabuni hapo Arsenal licha ya kudaiwa kueleza kuwa anataka kuondoka. Mirror.

No comments

Powered by Blogger.