Simba kuanza mazoezi leo Chuo cha Polisi Kurasini
DAR ES SALAAM- TIMU ya
soka ya Simba, inatarajiwa kuanza rasmi mazoezi ya kujifua kwa ajili ya msimu
ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi kilichopo
Kurasini jijini hapa.
Hayo yanajiri siku
chache, baada ya kuwasili kwa Kocha wa timu hiyo, Joseph Omog (pichani) kutoka kwao
Cameroon alikokuwa kwenye mapumziko ya baada ya kuisha kwa ligi hiyo maarufu
VPL.
Kocha huyo,
anaamini amerejea nchini kwa kazi moja tu ya kuhakikisha anakisuka upya kikosi
hicho ili msimu ujao kiweze kufanya vizuri katika michuano ya ligi kuu na ile
ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Akizungumzia
usajili wa timu hiyo, Omog amesema kuwa ni mzuri na wachezaji wote
waliosajiliwa mpaka sasa anawajua, hivyo kazi kubwa aliyonayo ni kuwaunganisha
ili waweze kucheza kitimu.
Chanzo;
Bongo5
No comments