Upinzani wamtaka Mugabe ang’atuke madarakani

HARARE-
VYAMA vya upinzani nchini, vimemtaka Rais Robert Mugabe (93) ajiuzulu, na
kumlaumu kwa kuiongoza nchi kutoka hospitalini kufuatia madai kuwa alisafiri kwenda
Singapore kwa matibabu.
Kwa mujibu Msemaji
wa chama kikuu cha upinzani cha MDC, Obart Gutu, vyama hivyo vinamtaka kiongozi
huyo ajiuzulu kwani hawezi tena kwenda sanjari na mikiki mikiki ya uongozi.
Akizungumza na
gazeti la binafsi la News Zimbabwe, Gutu alisema kwamba; “”Yeye si kijana tena
kwani umri umeshamtupa mkono. Kuendelea kuwepo madarakani, ni sawa na
kujiadhibu kwani hali yake si nzuri kimwili na kiakili.”
“Mugabe ni
lazima aondoke na aiache Zimbabwe iweze kusonga mbele chini ya uongozi mpya.”
Kwa upande
wake, Karauone Chihwayi, ambaye ni msemaji wa upande uliojitoa MDC alisema
kwamba; “Nchi imekwama leo hii kwa sababu Rais wa Zanu anaongoza akiwa kitandani
hospitalini.”
Chama cha
Zanu-PF kimemteua Mugabe kuwania urais mwaka ujao, licha ya kuonekana kutokuwa
na afya nzuri na amekuwa madarakani tangu mwaka 1980.
BBC
No comments