Header Ads

Ngeleja arudisha fedha za Escrow Serikalini



http://www.theworldfolio.com/img_db/timthumb.php?src=img_db/old/13226688671.jpg&w=800&z=1
DAR ES SALAAM- MBUNGE wa Sengerema, William Ngeleja amerejesha Serikalini (TRA) kiasi cha sh milioni 40.4 ambazo ni za mgawo wa Escrow aliopewa na mmiliki wa kampuni ya VIP Engineering, James Rugemalira.

Ngeleja (pichani) alisema ingawa alipewa fedha hizo kama sehemu ya msaada, ameamua kurudisha fedha hizo ili kukwepa kashfa hiyo ya ESCROW
“Fedha hizo nilizipokea kwa nia njema kama msaada kutoka kwa ndugu yangu Rugemalira, ili zinisaidie katika majukumu yangu ya kibunge na kutekeleza shughuli za kijamii kama vile ujenzi wa makanisa, misikiti na kulipia karo za wanafunzi,”
“Vile vile, nilipokea fedha hizo ili zinisaidie katika kutekeleza shughuli za kibunge ambazo hazipo katika bajeti ya Serikali. Nilipokea Fedha hizo bila kujua kwamba fedha hizo zilikuwa zinahusishwa na kashfa ya akaunti ya fedha za Escrow kama ilivyo sasa,”
“Nilipokea msaada huu kama wapokeavyo wabunge wengine, kwa nia njema. Nimepima na kutafakari, na hatimaye nimeamua, kwa hiari yangu mwenyewe, kurejesha kiasi cha Milioni 40.4 Serikalini (TRA),” alisema Ngeleja
Mbunge huyo alipewa mgao huo wa fedha kiasi cha milioni 40.4 na Rugemalira kupitia Benki ya Mkombozi mnamo Februari 12, 2014.
Chanzo; EATV

No comments

Powered by Blogger.