Header Ads

Sikumwambia baba lolote kuhusu mkutano na wakili – Trump Junior



https://thenypost.files.wordpress.com/2016/07/gop_2016_convention6.jpg?quality=90&strip=all&w=664&h=441&crop=1
WASHINGTON DC- MTOTO wa kiume wa Rais Donald Trump, amesema kuwa hakumfahamisha baba yake kuhusu mkutano na wakili raia wa Urusi ambaye alisema kuwa angesaidia katika kampeni yake ya uchaguzi.

Donald Trump junior alikiambia kituo cha habari cha Fox News kuwa, mkutano huo haukuhusu chochote.
Katika hatua nyingine, Trump Junior alitoa barua pepe zake zikionesha kuwa alikaribisha ombi la kukutana na wakili, ambaye alikuwa na uhusiano na Urusi, mwenye ujumbe potofu kuhusu Hillary Clinton.
Maofisa wa Marekani wanachunguza madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani. Tangu achaguliwe, Rais Trump ameandamwa na madai kuwa Urusi ilijumu kampeni ya Clinton.
Hata hivyo, Trump amekuwa akikana kufahamu lolote na Urusi mara kwa mara imekana kungilia kampeni hizo.
Alipoulizwa ikiwa alimwambia baba yake kuhusu mkutano wa mwaka uliopita, Trump Junior alisema hakukuwa na chochote cha kumwambia.
Donald Trump Junior, mkwe wa Trump, Jared Kushner na mwenyekiti wa kampeni Paul Manafort, walikutana na wakili wa Urusi, Natalia Veselnitskaya, katika jumba la Trump Tower mjini New York mnamo Juni mwaka 2016.
BBC

No comments

Powered by Blogger.