Header Ads

Mchakato wa nani atachapa karatasi za uchaguzi hautuhusu Jubilee- Ruto



We leave IEBC to decide who prints ballot papers - Jubilee
NAIROBI- NAIBU Rais nchini, William Ruto amesema kwamba, chama cha Jubilee hakitashiriki kwenye mikutano yoyote itakayoandaliwa na Tume Huru ya Uchaguzi (IEBC) ambayo itahusiana na mustakabali wa kampuni gani ipewe zabuni ya kuchapisha karatasi za kupigia kura.

Hayo yanajiri siku chache, baada ya Mahakama ya Rufaa nchini kusitisha zabuni ya uchapaji karatasi hizo ambayo awali ilitolewa kwa kampuni ya Al Ghurair ya Dubai, na kuiagiza IEBC ibainishe kampuni nyingine itakayochapa karatasi hizo.
Akizungumza jana kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Olenekenyu mjini Narok, Ruto alisema suala la nani atachapa karatasi hilo haliwahusu Jubilee ila ziwepo tu hapo siku ya uchaguzi huo Agosti 8 mwaka huu na kuongeza kuwa hawana ujuzi wala wataalam wa kuchapa karatasi hizo.
“Hatuna ujuzi huo wa kuchapa karatasi za kupigia kura. Tunaiachia IEBC mchakato mzima wa kutafuta kampuni ya kuchapa. Kwetu sisi Jubilee, tutakuwa tukiwasubiri wapinzani wetu hiyo Agosti 8, na kuwashinda warudi zao makwao,” alisema Ruto.
Aidha, Ruto alitumia fursa hiyo kuwataka wapinzani waache kutoa vitisho kwa tume ya uchaguzi vyenye nia ovu na kusema idadi ya kesi zilizofunguliwa na wapinzani dhidi ya IEBC, zinalenga kuahirisha uchaguzi kwa kutumia mahakama.
“Sisi Jubilee, tunataka kuwaambia NASA kuwa Wakenya wako tayari kupiga kura hiyo Agosti 8, 2017 na wala si tarehe na siku nyingine. Wamekuwa wakifungua kesi moja baada ya nyingine mahakamani, ili kuhujumu uchaguzi,” alisema Ruto.
Citizen Digital.

No comments

Powered by Blogger.