Rooney asema anaisubiri kwa hamu ziara ya Tanzania

LIVERPOOL- NYOTA
wa soka wa Uingereza, Wayne Rooney, ambaye amekamilisha uhamisho wake kutoka
Manchester United na kurejea Everton, amesema anasubiri kwa hamu kubwa kuzuru
Tanzania.
“Naisubiri
sana kwa hamu na ghamu (safari ya kwenda Tanzania) - naamini kuwa itakuwa safari
nzuri. Itakuwa nzuri sana na natumai kwamba nitaweza kuingia uwanjani na
kucheza.
“Huwa vizuri
sana unaposafiri na timu. Ni vizuri kuwa hotelini na wachezaji, kujumuika nao
na kuwafahamu zaidi. Sijawahi kwenda Tanzania, hivyo nasubiri sana kwenda huko,”
alisema Rooney.
Rooney
atakuwa kwenye kikosi cha Everton kitakachocheza mechi ya kujiandaa kwa msimu
ujao Tanzania. Amesema ziara hiyo, itampa fursa mwafaka ya kufahamiana na
wachezaji wenzake wapya.
Rooney
anayeongoza kwa ufungaji mabao Uingereza, alitia saini mkataba wa miaka miwili
Goodison Park Jumapili. Rooney alifika mazoezini
USM Finch Farm leo Jumatatu na anapangiwa kuungana na wenzake kwa safari hiyo
ya Tanzania baadaye wiki hii.
No comments