Header Ads

Rais Bouteflika aitaka Ufaransa iiombe radhi Algeria



ALGIERS- RAIS Abdelaziz Bouteflika kwa mara nyingine ameitaka mkoloni Ufaransa iiombe radhi rasmi Algeria, kutokana na jinai kubwa ilizowafanyia wananchi wa Algeria wakati wa utawala wa kikoloni.

Bouteflika alisema hayo jana, wakati wa maadhimisho ya miaka 55 ya uhuru na kusisitiza kuwa, Waalgeria wanaitaka Ufaransa iwaombe radhi kutokana na ukatili, mateso na masahibu yaliyosababishwa na taifa hilo wakati wa utawala wake wa kikoloni kwa miaka 132.
Hayo yanajiri katika kipindi ambacho Ufaransa ina Rais mpya, Emmanuel Macron, ambaye awali kabla ya kushinda kiti hicho alishawahi kuitembelea Algeria na kukiri kuwa ukoloni uliliathiri kwa kiasi kikubwa taifa hili.
Macron ambaye aliitembelea Algeria mnamo Februari mwaka huu, wakati alipokuwa anagombea urais wa Ufaransa, alikiri ukoloni wa nchi yake uliofanyika katika miaka ya kuanzia 1830 hadi 1962 ilikuwa ni jinai dhidi ya binadamu.
Zaidi ya watu milioni moja nchini, waliuliwa na wakoloni katika vita vya ukombozi.
Pars Today

No comments

Powered by Blogger.