Mwanamuziki mkongwe afariki Dar es Salaam

Mwanamuziki mkongwe
nchini, Shaaban Dede amefariki dunia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili
alikokuwa amelazwa kwa matibabu, kwa takriban wiki mbili.
Habari zilizothibitishwa
na mtoto wa nguli huyo, Hamad Dede, zimeeleza kuwa baba yake alifariki leo saa
mbili asubuhi hospitalini hapo.
Hamad alisema mipango
ya maziko inafanyika nyumbani kwa marehemu Mbagala, na ratiba na taratibu zote
zitatangazwa mara zitapokamilika kupangwa.
Marehemu Dede atakumbukwa kama mmoja wa wanamuziki nguli kutokea nchini Tanzania, kwa sauti yake tamu na utunzi wa nyimbo mbalimbali zilizoshika chati akiwa na bendi mbalimbali zikiwemo Tabora Jazz, Bima Lee, Mlimani Park na Mondo Ngoma ambako alikuwa anatumikia hadi maiti yamemkuta.
Marehemu Dede atakumbukwa kama mmoja wa wanamuziki nguli kutokea nchini Tanzania, kwa sauti yake tamu na utunzi wa nyimbo mbalimbali zilizoshika chati akiwa na bendi mbalimbali zikiwemo Tabora Jazz, Bima Lee, Mlimani Park na Mondo Ngoma ambako alikuwa anatumikia hadi maiti yamemkuta.
Jamii Forum
No comments