Header Ads

Pacquiao ataka video ya pambano lake na Horn ipitiwe upya



Many fans felt Pacquiao was unfairly stripped of his WBO Welterweight belt.
MANILA- MKALI wa ngumi nchini, Manny Pacquiao ameunga mkono hoja zinazoenea mitandaoni za kutaka kufanyike kwa mapitio ya video ya pambano la ngumi baina yake na Muasutralia, Jeff Horn.

Pambano hilo lililopigwa Jumapili iliyopita, liliibua utata kutokana na Horn kupewa ushindi na majaji wote watatu licha ya kuonekana kupigwa ngumi nyingi zaidi.
Jeff Horn of Australia fights Manny Pacquiao of the Philippines during the World Boxing Organization bout at Suncorp Stadium in Brisbane on July 1, 2017.
Jeff Horn
Akitoa taarifa yake kama Seneta, Pacquiao amesema anaunga mkono mwito wa chama cha ngumi nchini (GAB), ambacho kinataka kufanyika kwa mapitio ya video hiyo ili kubaini nani mshindi halisi.
“WBO inatakiwa ichukue hatua stahiki kuhusiana na barua iliyotumwa kwao na GAB, ili kuepusha kumomonyoa maadili ya mchezo na matakwa ya wapenda mchezo huo” ilieleza taarifa ya Pacquiao.
Aidha, taarifa hiyo ilieleza kuwa bondia huyo alikubali maamuzi hayo lakini akiwa kiongozi na mpiganaji ngumi, hana budi kudumisha na kupambana kwa ajili ya upatikanaji wa haki, uwazi na usawa kwa ajili ya umma.
“Ninaupenda mchezo wa ngumi na sipendi kuuona ukifa, kwa sababu ya maamuzi mabovu kutoka kwa maofisa wake,” ilieleza taarifa hiyo.
CNN

No comments

Powered by Blogger.