Header Ads

Putin na Jinping wapinga ufungwaji wa mtambo wa THAAD Korea Kusini



MOSCOW- RAIS Vladimir Putin na mgeni wake, Xi Jinping wa China, wamepinga ufungaji wa mitambo ya kutungua makombora wa Marekani (THAAD) ambao umefanyika nchini Korea Kusini.

Aidha, kwa viongozi hao kwa pamoja wamekubaliana kuendeleza uhusiano baina ya China na Urusi baada ya kukutana mjini hapa sanjari na kuongeza juhudi zao kutatua mgogoro wa Korea Kaskazini.
Hayo yalijiri jana baada ya viongozi hao kukutana katika Ikulu ya Kremlin mjini hapa, mara baada ya kuwasili kwa kiongozi huyo wa China na kufanya mazungumzo rasmi ikulu.
Kwa muda mrefu, China imekuwa ikidai kuwa mitambo hiyo ya THAAD ambayo imekuwa ikifungwa Korea Kusini, inachochea vurugu kwenye rasi hiyo ya Korea na pia inaipeleleza China.
CNTV

No comments

Powered by Blogger.