Pakistan yaanza mashambulizi dhidi ya Islamic State
ISLAMABAD- WANAJESHI
wa Pakistan, wameanzisha operesheni kubwa ya kijeshi dhidi ya wapiganaji wa
Islamic State (IS) katika mkoa wa Kaskazini Magharibi, ulio karibu na mpaka wa
Afghanistan.
Msemaji wa
Jeshi nchini, amesema kwamba wapiganaji hao wenye itikadi kali wamejiimarisha
ndani ya Afghanistan na hivyo wanapaswa kuzuiwa kufanya hivyo ndani ya
Pakistan.
Operesheni
hiyo inalenga zaidi kufanywa katika mkoa wa mpakani, huku ikiungwa mkono na
jeshi la Anga la Pakistan.
Serikali imekuwa
ikikanusha uwepo wa kundi hilo la IS ndani ya nchi, licha ya mfululizo wa
mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na kundi hilo katika kipindi cha miaka miwili
iliyopita.
No comments