Korea Kusini yataka mazungumzo ya kijeshi na Korea Kaskazini
BERLIN- KOREA
Kusini imependekeza kufanyika kwa mazungumzo ya kijeshi na Korea Kaskazini,
baada ya majuma kadhaa ya msukosuko, inayotokana na taifa hilo kufanya
majaribio ya mara kwa mara ya makombora yake.
Ikiwa
mazungumzo hayo yatafanyika, yatakuwa ndiyo ya kwanza ya juu kufanyika tangu
mwaka 2015.
Maofisa wa
vyeo vya juu Korea Kusini, wamesema kuwa mazungumzo hayo yatalenga kisitisha
vitendo vyote ambavyo huchangia kuwepo kwa misikusuko ya kijeshi katika eneo
lenye ulinzi mkali kati ya Kusini na Kaskazini.
Rais wa
Korea Kusini, Moon Jae-in tangu mwanzo alikuwa ameashiria kuchukua hatua ya
kuleta ushirikiano wa karibu na Korea Kaskazini.
Akihutubia
hivi karibuni mjini hapa, Jae-in alisema mazungumzo na Korea Kaskazini
yanastahili kufanyika na kutaka mwafaka kuafikiwa.
Lakini,
hatua za Korea Kaskazini kuyafanyia majaribio makombora likiwemo la hivi karibuni
la masafa marefu, yanaenda kinyume na maazimio ya Umoja wa Mataifa.
Naibu Waziri
wa Ulinzi wa Korea Kusini, Suh Choo-suk, aliwaambia wanahabari kuwa, mazungumzo
yatafanyika eneo la Tongilgak, katika jengo la Korea Kaskazini katika eneo
lisilo na ulinzi mkali kati ya nchi hizo mbili.
BBC
No comments