Header Ads

Pacquiao amepigwa kihalali- majaji



Horn took the title with a unanimous points win in Brisbane
BRISBANE- MATOKEO ya pambano la ngumi kati bondia maarufu duniani na mwanasiasa wa Ufilipino, Manny Pacquiao, na mwalimu Jeff Horn wa Australia yamebaki kama yalivyokuwa hapo awali.

Uamuzi huo umetoka baada ya majaji watano kutoka sehemu mbalimbali duniani, ambao waliitwa na Chama cha Ngumi cha WBO kutoa maamuzi hayo ambayo ni pigo kwa Pacquiao ambaye alidai kuwa mpinzani wake alipendelewa.
Mara baada ya Pacquiao kuomba mapitio hayo, WBO iliitisha majaji hao ambao walikaa kwa muda ambao haujawekwa wazi ili kupitia video hiyo bila sauti na kubaini kuwa Pacquiao alishinda raundi tano wakati Horn alishinda raundi saba.
Kwa matokeo hayo, ushindi wa Horn ambao awali ulisitishwa hadi maamuzi ya majaji hao yatoke, umerudishwa kama ilivyokuwa awali.
Aidha, WBO ilisisitiza kuwa uchunguzi huo ulifanyika kwa minajili ya kuongeza uwazi kwenye michezo hiyo na kukomesha dalili zozote za ulaghai na uonevu.
BBC Sport.

No comments

Powered by Blogger.