Header Ads

Mtoto wa Trump azidi kuandamwa Marekani



Donald Trump Jr at Trump Tower in New York City, 18 January 2017
NEW YORK- MTAYARISHAJI wa mkutano baina ya wakili wa Urusi, na Donald Trump Junior, Rob Goldstone ameeleza kuwa mtoto huyo wa kiume wa Rais Donald Trump, alielewa dhumuni la mkutano huo.

Hayo yanajiri muda mfupi, baada ya Trump Junior kuvifokea vyombo vya habari kwa madai ya kupotosha kile alichokizungumza juzi na kudai kuwa hakuwa akifahamu lolote kuhusu mkutano huo.
Kwa mujibu wa barua pepe ambayo gazeti la New York Times iliipata kutoka kwa Goldstone, Trump Junior alifahamishwa vema kuwa mkutano huo utahusu barua pepe za Hilary Clinton na si kama anavyodai yeye.
Gazeti hilo limeripoti kuwa, watatu hao walikutana huku wakifahamu kila kitu na barua pepe hiyo ya Goldstone ilibainisha kuwa Serikali ya Urusi ndiyo chanzo kikuu cha kuvuja kwa barua pepe za Clinton.
Lakini, gazeti hilo limeandika kuwa hakukuwa na maelezo yoyote yale kuhusu namna gani Urusi iliingilia uchaguzi huo wa mwaka jana na kumsaidia Trump kuingia madarakani.

No comments

Powered by Blogger.