Header Ads

Mwanaume atekwa na kubakwa na wanawake watatu Zimbabwe



http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2017/07/11/08/4236EA3F00000578-0-image-a-1_1499759421758.jpg
Kijiji cha Makoni
HARARE- MWANAUME mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 39, amelazwa katika hospitali ya Waza jijini hapa, baada ya kuvamiwa na kutekwa, kunyweshwa dawa za kulevya, kabla ya kufanyishwa mapenzi bila ridhaa yake na kisha kutupwa pembezoni mwa barabara kuu.

Inadaiwa kuwa tukio hilo limetekelezwa na kundi la wanawake, ambalo limekuwa likijihusisha na utekaji na ubakaji wa wanaume na kwenda kuwafanyisha mapenzi na kukusanya manii yao.
Madaktari wa hospitali ya Waza ambako mwanaume huyo ambaye anadaiwa kutoka kijiji cha Makoni, wilayani Chitungwiza amelazwa kwa ajili ya matibabu, wamethibitisha kuwa mwanaume huyo amefanyiwa ukatili wa kijinsia na wanawake hao.
Mara baada ya kuzinduka na kupata uwezo wa kuzungumza, mwanaume huyo amewaambia maofisa wa polisi kwamba alivamiwa na wanawake hao ambao walikuwa wakitumia gari aina ya BMW la bluu lenye namba za usajili za Afrika Kusini.
“Walikuwepo wanawake watatu kwenye gari hilo wakati nilipoambiwa nipande wakati nilipokuwa nikisubiri basi kituoni mnamo Julai 2, mwaka huu. Mara baada ya kupanda, nilipewa kinywaji na baada ya kunywa nilianza kujisikia kizunguzungu,”
“Baada ya hapo niliamka siku nyingine, nikajikuta nikiwa kwenye chumba kidogo chenye giza totoro. Nililazimika kujikagua na ndipo nilipojikuta nikiwa sina fedha kiasi cha dola za Marekani 120 (sh 264,000) nilizokuwa nazo na pia nilikuwa na michubuko kwenye kiungo change cha uzazi” anasema mwanaume huyo.
Baada ya kujikagua na kubaini kuwa na michubuko hiyo, mwanaume huyo alisema punde si punde wanawake hao walikuja tena chumbani hapo na kumtaka afanye nao mapenzi.
Anaeleza kwamba baada ya kutakiwa kufanya nao mapenzi, aliwakatalia na ndipo mmoja wa wanawake hao alitoa bastola na kumnyooshea huku akitishia kumpiga risasi na kumuua huku akimfunga mikono.
Mara baada ya kufungwa mikono, wanawake hao walitoa kinywaji kimoja na kumlazimisha mwanaume huyo anywe na kisha mmoja wao akaanza kuvua nguo na kumlazimisha mwanaume huyo afanye naye mapenzi.
“Baada ya kulazimishwa kunywa kile kinywaji, mwanamke wa kwanza alivua nguo zake na kunilazimisha kufanya naye mapenzi. Baada ya hapo mwingine naye alinibaka bila kutumia kinga, licha ya wenzake kumuomba asifanye hivyo bila kinga,” mwanaume huyo amewaambia polisi.
Mnamo Julai 4 mwaka huu, wanawake hao walimvisha mateka wao kinyago cha kufunika uso na kisha kumlazimisha kuingia kwenye gari na kwenda kumtupa kando kando ya barabara kwenye kijiji cha Muruta.
Baada ya kutupwa kando kando wa barabara, mpita njia mmoja alimuona mwanaume huyo na kisha kutoa taarifa polisi ambao nao walifika eneo hilo na kumkimbiza hospitalini.
tukio hilo la kutekwa na kubakwa kwa wanaume nchini, linaelezwa kuwa si la kwanza kutekelzwa na genge la wanawake hao wanaodaiwa kusaka manii ya wanaume.
Wanawake hao wamekuwa wakitekeleza utekaji huo na kisha kuwafanyisha mapenzi wanaume pasina ridhaa zao na kisha kukusanya manii ambazo huziuza kwa wahitaji ambao hawafahamu kuwa zimekusanywa kwa njia zisizo halali.
Polisi wanaendelea na uchunguzi ili kuwabaini wanawake hao na wameitaka jamii iwe macho, kwani matukio hayo yamekithiri.
Mail Online






No comments

Powered by Blogger.