Nitamtwanga Mayweather raundi nne za awali- McGregor

LOS ANGELES-
BONDIA Conor McGregor ameahidi kumtwanga mpinzani wake, Floyd Mayweather ndani
ya raundi nne za awali watakapokutana mnamo Agosti 26, mwaka huu.
McGregor
alisema hayo wakati wawili hao walipokutana kwa ajili ya kulizungumzia pambano
lao la Agosti 26. Wametokea mbele ya maelfu yamashabiki wao katika mkutano na
waandishi wa habari mjini Los Angeles.
“Upinzani
atakaoupata kutoka kwangu hajawahi kuupata kamwe, nitamtwanga ndani ya raundi
nne za mwanzo tu” alisema McGregor, 28.
Baada ya
tambo za McGregor, Mayweather alimjibu kwamba; “Nakuhakikishia nitaharibu uso
wako.” Mpambano huo unatajwa kuwa miongoni mwa itakayovutia zaidi duniani.
No comments