Header Ads

Lunch Time; Keita alike jezi ya Liverpool # Morata ndani Madrid # Ozil ataka £350,000 mkataba mpya Arsenal



http://www.footmercato.net/images/a/naby-keita-a-la-cote-en-europe_197049.jpg

LONDON- KIUNGO anayewindwa wa timu ya RB Leipzig na Liverpool, Nabil Keita, amedaiwa kutoa kiashiria muhimu kinachoonesha kwamba anataka kukipiga Anfield. Keita anadaiwa ku ‘like’ picha iliyowekwa mitandaoni inayomuonesha akiwa na jezi nyekundu ya Liverpool. Liverpool Echo.
http://cdn.images.dailystar.co.uk/dynamic/58/photos/875000/620x/Alvaro-Morata-621310.jpg
Windo la Chelsea, Alvaro Morata, anadaiwa kuwepo kwenye orodha ya wachezaji wa Real Madrid ambao wanaenda kwenye ziara Marekani. Morata (24) anatarajiwa kuwaonesha Man United makali yake watakapokutana hivi karibuni mjini Los Angeles. ESPN.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/10/bbbb-e1476919848408.jpg?w=960&strip=all 
Mesut Ozil amedai kuwa anataka kubaki Arsenal na anategemea kutia saini mkataba mpya na washika bunduki hao wa London. Mjerumani huyo amebakiza mwaka mmoja kwenye wake na anataka alipwe pauni 350,000 (sh bilioni 1.02) kwa wiki. Daily Mail.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/12/nintchdbpict0002874726314.jpg?w=960&strip=all
Kampuni za kuchezesha Kamari, zimeripotiwa kupunguza dau lao waliloweka kuhusu uwezekano wa Alexis Sanchez kujiunga na Ma City. Mchezaji huyo amekuwa akihusishwa mara kwa mara kuhama klabuni hapo. Manchester Evening News.
https://static.standard.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2016/09/11/21/kyle-walker.jpg
Dau la Man City kwa ajili ya kumsajili mlinzi wa pembeni wa Tottenham Hotspurs, Kyle Walker, linadaiwa kuwa pungufu kwa takribani pauni milioni 10 (sh bilioni 29). Walker anadaiw akuwa na thamani ya pauni milioni 50 (sh bilioni 145). Evening Standard.
http://i1.manchestereveningnews.co.uk/incoming/article4002162.ece/ALTERNATES/s1227b/158391643.jpg
Kocha wa West Brom Albion, Tony Pulis anadaiwa kutaka kuwasajili kwa mkupuo wachezaji wawili wa Man United, Chris Smalling (27) na Phil Jones (25). Wachezaji hao wamebakiza miaka miwili kila mmoja kwenye mikataba yao. Daily Mail.
http://1tvs492zptzq380hni2k8x8p.wpengine.netdna-cdn.com/wp-content/uploads/2017/07/GettyImages-644318626.jpg
Everton wanaweza wakaikosa huduma ya beki wa Uholanzi na Ajax, Jairo Riedewald (20), ambaye tayari Ajax imeshafikia makubalini na Crystal Palace. Daily Post.

No comments

Powered by Blogger.