China kuweka kambi ya jeshi Djibouti

DJIBOUTI
CITY- MELI zinazowasafirisha wanajeshi wa China kuja nchini, kuweka kambi ya Jeshi
ya China ambayo ndiyo ya kwanza ya kigeni kwa taifa hilo.
China
inasema kuwa, kambi hiyo itatumiwa kwa huduma za kulinda amani na za kibinadamu
Afrika na Magharibi mwa Asia.
Pia
itatumiwa kwa ushirikiano wa kijeshi, mazoezi ya kijeshi na huduma za uokoaji. China
imewekeza katika nchi za Kiafrika, na pia imeboresha kwa haraka jeshi lake
miaka ya hivi karibuni.
Shirika la
habari ya Xinhua lilisema kuwa, meli hizo ziliondoka bandari ya Zhanjiang
katika mkoa wa Kusini wa Guangdong jana lakini halikutaja idadi ya wanajeshi au
meli zilizoplelekwa Djibouti au ni lini kituo hicho kitaanza kutangaza huduma
zake.
Xinhua lilisema
kuwa kituo hicho cha Djibouti, kinabuniwa kufuatia mazungumzo kati ya nchi hizo
mbili. Kituo hicho kinaonekana kama hatua ya China ya kuwa na usemi wa kijeshi
eneo hilo.
BBC
No comments