Header Ads

Urusi yatishia kuwafukuza wanadiplomasia 30 wa Marekani



US President Donald Trump (R) speaks with Russian President Vladimir Putin at G20 in Hamburg, 7 Jul 17
MOSCOW- SERIKALI imesema iko tayari kuwatimua wanadiplomasia 30 wa Marekani na kutwaa mali za taifa hilo ikiwa ni hatua ya kujibu vikwazo ilivyowekewa na Marekani mwaka jana.

Kwa mujibu wa baadhi ya maofisa wa Serikali, vitisho hivyo vimetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi na kunukuliwa na gazeti la kila siku la Izvesta.
Desemba mwaka jana, utawala wa Rais Barrack Obama uliwatimua wanadiplomasia 35 wa Urusi na kufunga makao mawili ya kijasusi. Hatua hizo ni jibu kwa madai ya kuwa, Urusi iliingilia uchaguzi wa Marekani.
Urusi tayari iko chini ya vikwazo vya Marekani. Timu ya Rais wa sasa, Donald Trump nayo iko chini ya uchunguzi, kufuatia madai ya Urusi kuingia kati kampeni ya mwaka uliopita. Hata hivyo, Urusi imekana madai hayo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.