Mwanamke aitoroka familia kurudi kwa Boko Haram

BORNO- MWANAMKE
mmoja ambaye alikuwa ametekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram, amerudi kwa wapiganaji
hao kulingana na familia yake.
Aisha Yerima
mwenye umri wa miaka 25 alizungumza na Adaobi Tricia Nwaubani kabla ya kurudi
akisema; “Sasa nimeona kwamba vitu vyote ambavyo Boko haram walituambia
havikuwa vya ukweli. Sasa nikisilikiza katika redio, nacheka.”
Alisema hayo
baada ya kukamilisha mpango wa kumuondolea itikadi kali, lakini katika kipindi
cha chini ya miezi mitano baadaye, ameitoroka familia yake na kurudi kwa
wapiganaji hao.
Wakati
alipotekwa na wapiganaji hao, alikuwa ameolewa na kamanda ambaye alimfurahisha
kwa mapenzi na kumpa zawadi zenye thamani mbali na kumuimbia nyimbo za mapenzi
za Kiarabu.
Mwanasaikolojia
Fatima Akila, ambaye amefanya kazi na mamia ya wanawake waliookolewa, anasema mara
nyingine wanaonyesha kuwa na uwezo mkubwa.
“Hawa ni
wanawake ambao kwa kipindi kirefu hawakuwa wakifanya kazi, hawakuwa na uwezo,
hawakuwa na sauti katika jamii na mara moja wakaanza kuwasimamia kati ya
wanawake 30 jadi 100 ambao walikuwa chini ya udhibiti wao,” alisema Akila.
BBC
No comments