Jaji amfutia mashtaka mtu aliyemwita mbwa wake Buhari

Mkazi huyo
wa mji huu, Joachim Iroko ambaye ni mfanyabiashara, alikutwa hana hatia baada
ya waendesha mashtaka wa Serikali kushindwa kuweka wazi mashtaka hayo.
Iroko ambaye
awali alikamatwa na kuachiwa, alikamatwa tena na kufunguliwa mashtaka hayo
ambayo yalizua mkanganyiko na maandamano ya kupinga kuminywa kwa Katiba.
Kwa wakati
huo, Msemaji wa Rais Buhari, Garba Shehu alisema Rais Buhari alistaajabishwa na
hatua hiyo ya Iroko kumpa jina lake mbwa na kuongeza kuwa hatua hiyo
inadhihirisha ujinga wake (Iroko).
Akizungumza mara
baada ya kuondolewa mashtaka hayo, Iroko aliwashukuru wale wote waliokuwa wakimpigania
hadi kufikia hatua hiyo ya kuachiliwa huru.
Ilivyokuwa
Iroko anadaiwa
kutembea na mbwa wake mdogo, aliyekuwa ameandikwa jina la Buhari kwa rangi
kwenye pande zote za mbavu katika eneo wanaloishi watu wengi wanaomuunga mkono
Rais Buhari.
Polisi walisema
walilazimika kumkamata kutokana na kuhofia usalama wake, kwani wananchi
wanaweza wakamdhuru endapo akiendelea kuonekana.
Hata hivyo,
Iroko amekuwa akisisitiza mara kwa mara kuwa aliamua kumuita mbwa huyo jina
hilo kwani Rais Buhari ni shujaa wake na anapambana na ubadhirifu.
“Nilimwita
mbwa wangu kipenzi Buhari, kwani naye Rais Buhari ni shujaa wangu. Vitu
anavyovifanya vimenivutia na vinanipa hamasa zaidi,” alisema Iroko ambaye
aliviambia vyombo vya habari kuwa amepokea vitisho vya kuuliwa na watu
wasiojulikana.
BBC.
No comments