Header Ads

Mbivu mbichi za dhamana ya Lissu kujulikana kesho


IMG-20170724-WA0008.jpg

KESI ya uchochezi inayomkabili Mwanasheria Mkuu wa Chadema ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu itaendelea kesho katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, huku Wakili wake Fatma Karume akiwa na imani kuwa mteja wake atapewa dhamana.

Fatma amesema endapo Mahakama hiyo haitatoa dhamana kwa Lissu, watakata rufaa Makahama ya Rufaa.

Lissu anayetetewa na mawakili 18, anatuhumiwa kuwa Julai 17, akiwa mtaa wa Ufipa, Kinondoni alitoa lugha ya uchochezi hali ambayo ingesababisha chuki kwa sababu aligusa udini, ukabila na ukanda. 

Julai 24, Mbunge huyo alinyimwa dhamana na kutakiwa abaki rumande hadi kesho ambapo Mahakama itatoa uamuzi wa dhamana, kutokana na upande wa Jamhuri kuwasilisha pingamizi. 

Mahakama hiyo ilifikia uamuzi huo, baada ya mawakili wa Lissu, Fatma na wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi na Saimon Wankyo kujibizana kwa hoja kwa zaidi ya saa mbili.

Baada ya majibizano hayo, Hakimu Mkazi Wilbard Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi kesho ili apitie hoja hizo na kuziandikia uamuzi.

No comments

Powered by Blogger.