Header Ads

Wanasayansi New Zealand wagundua chanjo ya kisonono



Gonorrhoea imekuwa taabu kutibika kwa sababu imezoea antibiotic
WELLINGTON- WANASAYANSI nchini, wameonesha kwa mara ya kwanza kwamba chanjo maalum inaweza kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa kisonono.

Hayo yanajiri isiku chache, baada ya Shirika la Afya Duniani (WHO), kuonya kwamba ugonjwa huo wa kuambukiza kwa njia ya zinaa, umekuwa sugu dhidi ya dawa zake.
Watafiti kutoka chuo kikuu cha Auckland wamegundua kuwa, maambukizi ya ugonjwa huo wa zinaa yameshuka kwa takriban theluthi moja miongoni mwa watu ambao walipata chanjo dhidi ya homa ya manjano.
Watafiti hao, wamefuatilia kutoka kwa vijana milioni moja waliopata chanjo hiyo pindi kulipotokea ugonjwa wa homa ya manjano nchini.
Kisonono imekuwa sugu kutibika, kwa sababu kimezoea dawa za antibiotic. Mwandishi wa BBC wa masuala ya afya, anasema utafiti huu unaonesha inawezekana kuwa na chanjo dhidi ya ugonjwa.
BBC

No comments

Powered by Blogger.