Mtoto Bradley kuzikwa Ijumaa

LONDON- UNAMKUMBUKA
yule mtoto ambaye alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Saratani? Ni yule
aliyekuwa shabiki mkubwa wa Sunderland ya Uingereza.
Iko
hivi, mtoto huyo, Bradley Lowery ambaye alifariki wiki iliyopita, familia yake imetoa
utaratibu wa maziko ya mtoto wao yatakayofanyika Ijumaa na kuwataka
waombolezaji kuvaa fulana za soka ili kukumbuka miaka sita ya maisha yake.
Shabiki
huyo mkubwa wa Sunderland ambaye alijenga urafiki mkubwa na mchezaji kipenzi
chake, Jermain Defoe, alipoteza vita vyake na saratani adimu kwa watoto ijulikanayo
kama neuroblastoma Ijumaa.

Habari
yake iligusa nyoyo za watu duniani kote na alililiwa na mamilioni ya watu wakiwamo
maarufu.
Familia
hiyo jana ilitoa taarifa juu ya maziko yake ambayo yatafanyika kwenye Kanisa
Katoliki la Mt Joseph mjini Blackhall Colliery, Co Durham, Ijumaa ijayo.
Waliandika
kwenye ukurasa wa Facebook kwamba “saratani haina rangi” na watu wanavaa fulana
za soka kwa heshima ya mtoto wao.
Familia
hiyo pia ilikumbusha mashabiki wake, kwamba wanachanga fedha kwa ajili ya Wakfu
wa Bradley Lowery na waombolezaji wanaweza kutoa fedha kwa ajili hiyo kupitia
mkondoni.
Ujumbe
huo ulisema: “Hii iko wazi kwa kila mtu ambaye atapenda kuja na kusherehekea
maisha ya Bradley na kutoa heshima zao kumwonesha jinsi walivyompenda.
“Si
kila mtu ataweza kuingia kanisani lakini kuna vipaza sauti nje kwa ajili ya
watu kusikiliza misa na watu wanaweza kujipanga barabarani kama wataona inafaa.
“Baadaye
kutakuwa na mialiko kwenye sherehe ya faragha makaburini. Familia imeomba
kusiwe na vyombo vya habari isipokuwa kama wanahabari watakuwapo, si kikazi
bali kutoa heshima zao.
“Unaweza
kuvaa unavyotaka kwa ajili ya mazishi, lakini familia na marafiki wameamua kuja
na kaulimbiu ya saratani haina rangi. Hivyo watavaa mashati ya soka bila kujali
ni timu au rangi gani.
“Kutokana
na umaarufu wa Bradley, wangependa maua ya familia tu na kama utapenda
kuchangia hilo basi mchango uelekezwe kwenye Wakfu wa Bradley Lowery.”
Msichana
wa miaka minane, Brooklyn Hutchinson, ambaye naye anapambana na saratani,
alipatwa mshituko mkubwa aliposikia kifo cha Bradley. Alijenga uhusiano imara
na Bradley, kwani walikuwa wakipata tiba ya kemikali pamoja.
Mara
nyingi walionekana wakitembea pamoja kwenye kitengo cha saratani cha hospitali
ya Royal Victoria, Newcastle.
Mama
yake Brooklyne, Joanne, alieleza jinsi binti yake alivyopata pigo baada ya
kusikia taarifa za kifo cha Bradley.
Aliiambia
Daily Mirror: “Ilisikitisha sana. Aliniuliza, ‘inawezekanaje Bradley afe? Ana
miaka sita tu’.
“Walipenda
kucheza pamoja wodini na kuongozana kwenye chumba cha sanaa.
“Walikuwa
sawa na jozi yoyote ya watoto wanaofurahi pamoja shuleni. Wakati mwingine
wakiwa wanacheza na kucheka pamoja ungesahau matatizo waliyonayo.
“Nadhani
hicho ndicho pia kilikuwa kikitokea kwao. Fikra zao zilisahau matibabu na siku
zao ngumu.”
Brooklyn
aligundulika na saratani ya figo Agosti, 2015 na tiba ya kemikali
ilimsababishia kushindwa kutumia miguu na mikono yake kwa muda mfupi.
Alilazimika hata kuondolewa figo moja.
Januari
mwaka jana, alihakikishiwa kuwa tatizo limekwisha, lakini miezi sita badaye,
wazazi wake wakachanganyikiwa kubaini uvimbe mwingine kwenye pafu lake la
kulia. Baada ya kuondolewa pafu lake
Januari, hivi sasa anapata matibabu tena.
No comments