Header Ads

Mchezaji Manchester United ageukia Upadri



http://www.catholicherald.co.uk/content/uploads/2012/01/mulryne-800x500.jpg
BELFASTI- MIONGONI mwa watu wagumu na wakaidi wa kuishi maisha mengine nje ya soka, wacheza mpira. Wao huwa hawaamini kama kuna maisha kwingineko baada ya kutundika daluga zaidi ya kurudi kuwa makocha au wakurugenzi wa kiufundi au kumiliki akademi za mpira.

Lakini, hali ni tofauti kwa mchezaji wa zamani wa Manchester United, Philip Mulryne. Yeye amegeukia Upadri na mwishoni mwa wiki alipata daraja hilo na kufanikiwa kusalisha misa yake ya kwanza katika eneo alilozaliwa la Belfast, Ireland.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/10/sport-preview-philip-mulryne-new.jpg?strip=all&w=1200&h=800&crop=1
Padri Mulryne, ambaye aliwahi kuripotiwa kupata malipo ya pauni 600,000 kwa mwaka alipokuwa mwanasoka wa kulipwa, alirejea katika Parokia ya Mt Oliver Plunkett iliyopo Lenadoon siku mbili baada ya kupewa daraja la Upadri mjini Dublin na kusalisha misa yake ya kwanza Jumapili.
Padri Mulryne alianza kucheza soka katika timu ya soka ya parokia yake, St Oliver Plunkett.
Akiwa katika timu hiyo, alionwa na wasaka vipaji wa Manchester United, akiwa na umri wa miaka 14 na kualikwa kujaribiwa kisha alipewa mkataba wa miaka miwili.
Mwaka 1994, Padri Mulryne alipohitimu sekondari, alikwenda Manchester United na kuwa mwanasoka wa kulipwa kwa mkataba wa miaka minne, alicheza mechi yake kwanza ya kulipwa 1997 dhidi ya timu ya Ipswich Town.
Alicheza mechi tano katika timu ya United kabla ya kuhamishiwa Norwich City 1999.  Katika miaka sita aliyokuwa katika timu hiyo, alicheza mechi 135.
Aliichezea mechi ya kwanza timu ya Taifa ya Ireland Kaskazini mwaka 1997 dhidi ya Ubelgiji na kuichezea mechi 27 na kufunga mabao matatu.
Baada ya kuichezea kwa muda mfupi katika timu za Cardiff City na Leyton Orient, Padri Mulryne alistaafu kucheza soka mwaka 2009 na baadaye alijiunga na Seminari ya Diocesan ya Mt. Malachy iliyopo Belfast.
Kisha alisomea falsafa katika  Chuo Kikuu cha Queens na Chuo cha Maryvale kilichopo Birmingham na kuhitimu kabla ya kwenda Italia kusomea Theolojia katika Chuo Kikuu cha  Gregorian.
Alipewa daraja la upadri Jumamosi katika Kanisa la Mt Saviour mjini Dublin na Askofu Joseph Augustine Di Noia ambaye alimpongeza kwa kutimiza wito wake kwa kuamua kumtumikia Mungu baada ya kuwa mwanamichezo.
Daily Mail

No comments

Powered by Blogger.