Header Ads

Mkanyagano uwanjani waua watu 8 Malawi



https://malawi24.com/wp-content/uploads/2017/04/Bingu-National-Stadium.jpg
LILONGWE- WATU nane wakiwemo watoto saba na mtu mzima mmoja, wamekufa huku wengine zaidi wamejeruhiwa kwenye mkanyagano uliotokea kwenye uwanja wa taifa wa Bingu.

Taarifa ya polisi, imeeleza kuwa kanyagano huo umetokea baada ya mamia ya watu kusongamana wakati wakijaribu kugombania viti uwanjani hapo kwa ajili ya kuangalia mchezo wa kirafiki baina ya Nyasa Big Bullets na Silver Strikers.
Rais Peter Mutharika ametoa pole kwa wafiwa na familia zao kwa ujumla, na kuahidi kuwa Serikali itafanya kila liwezekanalo kusaidia familia hizo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.