Header Ads

Arsenal na Leicester kukipiga Agosti 11 # Everton yaanza ‘jeuri ya pesa’ # Leicester yanasa kiungo wa Sevilla



https://i0.wp.com/www.fullmatchesandshows.com/wp-content/uploads/2017/04/Arsenal-vs-Leicester-City.jpg?fit=600%2C300

LONDON- CHAMA cha Soka nchini (FA), kimerudisha nyuma mchezo wa Arsenal dhidi ya Leicester City, hadi siku ya Ijumaa ya Agosti 11, mwaka huu.
Mchezo huo wa ufunguzi, unatarajiwa kuchezwa majira ya 19:45 (kwa masaa ya Uingereza) huku michezo mingine ikibaki kuwa Jumamosi.
Agosti 12, 2017 *saa za Uingereza
Watford v Liverpool (12:30)
Brighton v Man City (17:30)
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/03/nintchdbpict000299479451.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Baada ya kupata uhakika wa fedha zilizotokana na kumuuza Romelu Lukaku kwa Man United, timu ya Everton imedaiwa kuanza mbio za kumsajili kiungo wa Swansea, Gylfi Sigurdsson (27). Lakini watalazimika kulipa pauni milioni 40 (sh bilioni 116) kuipata saini yake.
https://leicesterfc-static-files.s3.amazonaws.com/leicesterfc/photo/2017/07/06/86666b5f-8128-4205-8be3-1fb75974dbba/775002733-013.JPG
Klab ya Leicester City imetangaza kumsajili kiungo wa Sevilla, Vicente Iborra, kwa kiwango cha ada ambayo haijawekwa wazi.
Iborra aliuambia mtandao wa klabu hiyo kwamba; “Ninafuraha kujiunga na Leicester City na ninategemea kupata uzoefu mwingi kwenye ligi hii ya Premier League sanjari na wachezaji wenzangu.”
Zote na BBC Sport

No comments

Powered by Blogger.