Header Ads

Bunge la Upinzani lavamiwa Venezuela



Opposition lawmaker Luis Stefanelli (L) gestures next to fellow opposition lawmaker Leonardo Regnault after a group of government supporters burst into Venezuela's opposition-controlled National Assembly during a session, in Caracas
CARACAS- WATU wanaokadiriwa kufikia 100 ambao wanadaiwa kuwa wafuasi 100 wa Serikali, wamevamia Bunge linalodhibitiwa na Upinzani nchini na kuwapiga wabunge.

Mashuhusa wanadai kuwa, makabiliano hayo yalitokea baada ya Kikao cha Bunge kuadhimisha siku ya uhuru. Polisi waliokuwa wakilinda Bunge, walitazama wakati wavamizi waliokuwa na fimbo walipovunja lango lakini Serikali imeapa kufanya uchunguzi.
Kwa mujibu wa Spika wa Bunge, Julio Borges, watu 350 walifungiwa ndani ya bunge kwa saa kadhaa, wakiwemo waandishi wa habari, wanafunzi na wageni wengine.
Borges aliwataja wabunge watano waliojeruhuwa na kusema kuwa, baadhi walipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu. Venezuela imetikiswa na maandamano yenye ghasia miezi ya hivi karibuni, na sasa inakumbwa na matatizo ya kiuchumi.
Wizara ya Mambo ya Nje imelaani ghasia hizo, ikizitaja kuwa dhuluma dhidi ya demokrasia inayofurahiwa na watu wa Venezuela tangu ipate uhuru miaka 206 iliyopita
Kabla ya wavamizi kuingia kwenye majengo ya Bunge, Makamu wa Rais, Tareck El Aissami alionekana bungeni akiandamana na Mkuu wa Majeshi, Vladimir Padrino Lopez.
Inadaiwa kuwa mara baada ya kuondoka, El Aissami alitoa hotuba akiwashauri wafuasi wa rais kwenda bungeni kumuonesha rais uungwaji mkono. Umati mkubwa wa watu ulikuwa ukiandamana nje ya majengo ya bunge kwa saa kadhaa kabla ya kuingia ndani.
BBC

No comments

Powered by Blogger.