Header Ads

Mezani kwetu leo; Rooney aondolewa kwenye orodha Man United # Rudiger atua London kukamilisha usajili # Man United kufa kupona kwa Morata



Image result for wayne rooney

LONDON- NAHODHA wa Manchester United, Wayne Rooney, 31, ameondolewa kwenye orodha ya wachezaji wa timu hiyo wanaokwenda kwenye ziara nchini Marekani, ili aweze kukamilisha uhamisho wake wa kurudi katika klabu yake ya zamani ya Everton bure.
Pia, Everton imeonesha nia ya kumtaka mshambuliaji wa Arsenal na Ufaransa, Olivier Giroud kwa ada ya pauni milioni 20 (sh bilioni 58). The Sun
Image result for Ivan Perisic
Kwa upande wao, Man United wameripotiwa kufufua tena nia yao ya kumtaka winga raia wa Croatia anayekipiga Inter Milan ya Italia, Ivan Perisic (28) kwa dau la pauni milioni 48 (sh bilioni 139). Sky Italia
Image result for Alvaro Morata
Pia, gazeti la The Independent limeeleza kuwa Man United wanatarajiwa kuweka msukumo wa mwisho kwenye mpango wao wa kumnasa mshambuliaji wa Real Madrid, Alvaro Morata (24). Lakini inaripotiwa kuwa, Madrid wamekataa kata kata kushusha dau lao wanalotaka la pauni milioni 72 (sh bilioni 208.8).
Image result for Antonio Rudiger
Daily Mirror wameripoti kuwa mlinzi wa kati wa Roma, Antonio Rudiger (24) amewasili jijini London, kwa ajili ya kufanya vipimo na kukamilisha usajili wake kwenda Chelsea kwa dau la pauni milioni 36 (sh bilioni 104.4).
Image result for Alphonse Areola
Klabu hiyo ya London ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza, wameripotiwa kumtaka mlinda mlango wa PSG ya Ufaransa, Alphonse Areola (24). Daily Star.
Image result for Ross Barkley
Tottenham Hotspurs wameripotiwa kumtaka kiungo mshambuliaji wa Everton, Ross Barkley (23) ili kukiongezea nguvu kikosi chao lakini hawataki kulipa dau la pauni milioni 50 (sh bilioni 145) zinazotakiwa kama ada ya uhamisho. The Sun.   
Image result for Emanuel Mammana
Liverpool imeripotiwa kuweka mezani dau la pauni milioni 14.9 (sh bilioni 43.2), kama ada ya uhamisho ya mlinzi kinda kutoka Olympic Lyon ya Ufaransa, Emmanuel Mammana (21). Sport Review.
Image result for Kasper Dolberg 
Televisheni ya klabu ya Ajax, imeliambia Shirika la Habari la Goal.Com kwamba, windo la timu za Manchester United na Manchester City, Kasper Dolberg (19), hataki kuondoka klabuni hapo na kuelekea Old Trafford au Etihad.
Image result for Tim Krul
Kocha wa Newcastle United, Rafael Benitez, amewapa nafasi ya mwisho wachezaji wake, Tim Krul (29), Henri Saivet (26), Siem De Jong (28) na Emmanuel Riviere (27) ili kuonesha kiwango cha kumvutia kwenye michezo ya maandalizi ya msimu (Newcastle Chronicle).

No comments

Powered by Blogger.