Header Ads

Afrika Kusini yaendeleza nia yake ya kujitoa ICC



Image result for Omar Al Bashir
CAPE TOWN- CHAMA tawala nchini (ANC), kimeonesha kuwa bado kina mipango ya kuiondoa Afrika Kusini kwenye uanachama na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

ICC inatarajia kutangaza kesho iwapo Afrika Kusini ilivunja sheria kwa kushindwa kumkamata Rais wa Sudan, Omar al Bashir (pichani), alipofanya ziara nchini mwaka 2015.
Rais Bashir anashutumiwa kutekeleza mauaji ya kimbari wakati wa mzozo wa Darfur. Serikali ilikua na mipango hiyo tangu miaka miwili iliyopita.
Ilikua ni msukumo uliofanywa na baadhi ya Serikali za Afrika dhidi ya taasisi hiyo, zikidai kuwa ICC imekua ikilionea bara la Afrika na viongozi wake.
Mahakama Kuu nchini, yenyewe imesema Serikali imekua ikifanya mchakato huo kinyume na Katiba, ikishindwa kulipeleka suala hilo bungeni.
Pamoja na hayo ANC kimesema hakitarudu nyuma, wataendelea na mipango yao ya kujiondoa ICC.
BBC

No comments

Powered by Blogger.