Mezani Asubuhi; Bale njia nyeupe Man United # Conte amtaka Barkley # Liverpool yamkomalia Keita
![https://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2016/01/10/13/gareth-bale-23324.jpg](https://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2016/01/10/13/gareth-bale-23324.jpg)
Kocha wa Chelsea, Antonio Conte, ameandaa pauni milioni 50 (sh bilioni
145) kwa ajili ya kuwasajili wachezaji wawili wa Uingereza, Ross Barkley (23)
kutoka Everton na Alex Oxlade-Chamberlain (23) wa Arsenal. Sun.
Liverpool wako tayari kutoa ofa yao ya mwisho kwa RB Leipzig, yenye
thamani ya pauni milioni 70 (sh bilioni 203) na kipengele kitakachoruhusu
ongezeko ili kumnasa Naby Keita (22). Mirror.
![https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/05/686314800.jpg](https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/05/686314800.jpg)
Hatima ya usajili wa kiungo wa Liverpool, Philippe Coutinho (25) imezidi
kuingia shaka, baada ya Liverpool kueleza kuwa hawatabadili msimamo wao wa
kutomuuza mchezaji huyo licha ya kudaiwa kuelewana maslahi binafsi na
Barcelona. ESPN.
Juventus imekaribia kukamilisha usajili wa kiungo wa PSG, Blaise Matuidi
(30) na kujiondoa kwenye mbio za kumsajili kiungo wa Chelsea, Nemanja Matic
(28). Independent.
![https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict0003274565322.jpg?strip=all&w=960&quality=100](https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict0003274565322.jpg?strip=all&w=960&quality=100)
Mwenyekiti wa AC Milan, Marco Fassone amebainisha kuwa wamefanya
mazungumzo na wakala wa mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa (28) kwa ajili ya
kumsajili. Sky Sports.
![https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/05/nintchdbpict000321041525.jpg?strip=all&w=960&quality=100](https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/05/nintchdbpict000321041525.jpg?strip=all&w=960&quality=100)
Mshambuliaji wa Ufaransa na Real Madrid, Karim Benzema (29) anatarajiwa
kusaini mkataba mpya na Real Madrid bila kujali kama klabu hiyo itamsajili Mfaransa
mwenzake, Kylian Mbappe (18). Marca.
![https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/02/nintchdbpict000296232831.jpg?strip=all&w=960](https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/02/nintchdbpict000296232831.jpg?strip=all&w=960)
Mshambuliaji wa Juventus, Paulo Dybala (23) ambaye anawindwa na miamba
miwili, Manchester United na Barcelona, amesema hana mpango wa kuondoka
Juventus msimu huu. Talksport.
![https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/07/6329671261.jpg?w=748&h=498&crop=1](https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/07/6329671261.jpg?w=748&h=498&crop=1)
Bosi wa Inter Milan, Luciano Spalletti amesema angependa winga wa timu
hiyo, Ivan Perisic (28) abakie klabuni hapo lakini hawezi kusema jambo gani
litatokea siku za usoni. ESPN.
No comments