Iran yafanya jaribio la roketi ya kubeba satalaiti
![The Phoenix rocket is launched](https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/4CC2/production/_97105691_mediaitem97105690.jpg)
TEHRAN- IRAN
imefanikiwa kuifanyia jaribio roketi ambayo ina uwezo wa kupeleka satalaiti
hadi mzingo wa dunia, siku moja baada ya Marekani kuiwekea vikwazo vipya
kufuatia mpango wake ya kinyuklia.
Roketi hiyo
ya Phoenix, ilirushwa kutoka kituo kipya cha anga za juu kilicho Semnan, Kaskazini
mwa nchi. Marekani ililaani jaribio hilo na kulitaja kuwa kitendo cha uchokozi.
Hilo ni jaribio
la tano la roketi iliyoundwa nchini, tangu mwaka 2009. Televisheni ya taifa inasema
kuwa roketi hiyo, itabeba satalaiti ya uzito wa kilo 250 hadi umbali wa kilometa
500 angani.
Msemaji wa Wizara
ya Mambo ya Nje Marekani, anasema kuwa ikiwa itathibitishwa, jaribo hilo
linaweza kukiuka maazimio ya Baraza la Umoja wa Mataifa.
Iran iliapa
kujibu vikwazo vipya viivyotangazwa na Marekani, ambavyo vililenga makampuni 18
au watu ambao wameunga mkono programu za makombora za Iran.
Vikwazo
hivyo vipya, vilitangazwa siku moja baada ya utawala wa Trump kusema kuwa Iran
inatekeleza makubaliano ya mwaka 2015 ya kuachana na mpango wa kinyukia.
BBC
No comments