Bunge la Senate Marekani laridhia vikwazo Urusi, Iran na Korea Kaskazini
![https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/14A50/production/_97106548_gettyimages-810246808.jpg](https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/14A50/production/_97106548_gettyimages-810246808.jpg)
WASHINGTON
DC- BUNGE la Senate nchini, limepiga kura ya kuziwekea vikwazo vipya Urusi,
Iran na Korea Kaskazini licha ya pingamizi kutoka Ikulu ya White House.
Bunge la Wawakilishi
(Congress), liliidhinisha muswada huo mapema wiki hii kwa kura nyingi. Baada ya
muswada huo kupita katika mabunge yote, sasa utapelekwa kwa Rais Donald Trump
kuwekwa sahihi.
Lakini Trump
anataka kuboresha uhusiano na Urusi, na anaweza kuukataa licha na uungwaji
mkono uliopata. Vikwazo hivyo ni vya kuiadhibu Urusi zaidi, kufuatia hatua za
kulimega eneo la Crimea kutoka Ukraine mwaka 2014.
Lakini
mjadala kuhusu vikwazo hivyo vipya, unafanyika huku uchunguzi kuhusu hatua za
Urusi kuingilia kati uchaguzi wa Marekani wa mwaka 2016 ukiendelea.
Trump mara
nyingi amekana kuwa Urusi iliingilia uchaguzi huo kusaidia kampeni yake.
Waandishi wa
masuala ya siasa, wanasema ikiwa Trump atajaribu kuukataa muswada huo basi
itakuwa ishara tosha kuwa anaiunga mkono Urusi.
BBC.
No comments