Header Ads

Mchezaji wa Ajax akutwa na tatizo la kudumu la ubongo



http://www4.pictures.zimbio.com/gi/AFC+Ajax+v+Panathinaikos+FC+UEFA+Europa+League+L5lNVMFlgrKx.jpg

AMSTERDAM- SOKA limeendelea kutikiswa na matukio ya wachezaji kuanguka na kupoteza fahamu uwanjani, baada ya mchezaji wa Ajax, Abdelhak Mouri kuanguka na kuzimia ghafla kabla ya kuthibitishwa kapata tatizo la kudumu la ubongo.
Katika mchezo uliochezwa Jumamosi dhidi ya Werder Bremen ya Ujerumani, Nouri mwenye umri wa miaka 20 alianguka kutokana na kupatwa na tatizo mapigo ya moyo kutokuwa sawa.
Taarifa ya Ajax iliyotoka Jumatatu, ilieleza kuwa mara baada ya vipimo kufanyika, ilibainika kuwa moyo wake unafanya kazi kama kawaida na vipimo vya ubongo haukuonesha kuwa na tatizo.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa amepatwa na tatizo la kudumu la ubongo.
Taarifa hiyo imesema kwamba; “Maombi yetu yako kwake na kila mtu hapa Ajax na duniani kote, anamuombea (Nouri) apone. Familia yote ya wapenda soka, inafuatilia kwa ukaribu maendeleo yake kiafya.” 
BBC

No comments

Powered by Blogger.